HALMASHAURI YA JIJI LA DAR ES SALAAM YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KWA WAJASIRIAMALI WADOGO

Na.Khadija seif,Globu ya jamii

HALMASHAURI ya jiji la Dar es salaam lameadhimisha siku ya wiki ya utumishi wa umma kwa kutembelea viwanda vya wajasiliamali wadogo jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji Herman amesema Serikali Ina nia ya dhati kuwanyanyua wajasiLiamali hao kibiashara ili kukuza pato la taifa.

Wiki hii ya utumishi wa umma imeanza juni 17 na unatarajiwa kufika kilele juni 23 mwaka huu.Aidha, ameeleza WajasiLiamali hao wadogo na wanafanya shughul hizi katika mazingira shirikishi na halmashauri ikaamua kuwatengea wajasiriamali hao sehemu ya kuuza biashara hizo.

" Mpaka sasa vikundi 15 katika kata ya mwanayamala wamekua wanufaika wa mikopo iliyotengwa na serikali na million 853 imeshatolewa ,"Hata hivyo Serikali imeweka mikakati mizuri kuhakikikasha 10% ya mapato ya ndani zinatengwa kwa ajili ya kusaidia kundi maalum wakiwemo walemavu na wakina"

WajasiLiamali wameanzisha shughulI za uzalishaji wa usindikaji chakula ,sabuni. Mafuta,viatu , batik ushonaji na uchoraji.Kaimu Muhandisi wa halmashauri ya jiji Jumanne Manish amesema ujenzi ulizingatia maeneo ambayo ni rahisi kufikiwa kwa wahitajika. 

Pia Manish ameeleza kuwa ujenzi unaendelea kwenye jengo hilo kufatia wajasiriamali kuomba kuanza shughul zao kabla ya kukamilika matengenezo makubwa Kama kuleta umeme mahali hapo kwa wajasiriamali ambao shughuli zao zintegemea sana umeme.

"Uboreshwaji wa majengo utaendelea na tutegemee kuwepo kwa majengo ili kupanua wigo wa kibiashara na kutakuwepo jengo la utawala pamoja na wataalam watakaowezesha wajasiriamali kuhifadhi fedha ,"

Kwa upande wake mjasiriamali mdogo wa kiwanda cha batiki amewashukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John pombe Magufuli kwa kuona ipo haja ya kutenga fedha kwa ajili ya kundi maalum .

"Mimi ni mmoja wa wanufaika wa mikopo ya Serikali na imeniwezesha kununua vifaa vipya vinavonisaidia kushona kwa haraka zaidi tofauti na hapo awali nilikua natumia mashine ya kushonea ya kizamani,"

Amewaomba wakina mama kuchukua mikopo hiyo kwa ajili ya biashara na si vingine kutokana na ipo kwa ajili ya kunyanyua wakina mama na kupanua wigo wa kibiashara zaidi.

No comments: