MANYARA TANZANITE MARATHON 2026 YAENDESHA MBIO ZA HISANI, LENGO KUKUSANYA SHILINGI BILIONI 1.5

Manyara Tanzanite Marathon 2026, mbio za hisani zenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi na uwezeshaji wa wodi maalum ya kuwahudumia watoto njiti, zimefanyika leo katika Mji wa Babati, zikiwa na kaulimbiu “Hatua Moja, Okoa Maisha ya Mtoto Njiti.”

Mbio hizo za hisani zimeongozwa na Mgeni Rasmi kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mhe. Mwigulu Nchemba, Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Daniel Sillo, ambaye amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Manyara kwa ubunifu wa kuanzisha Manyara Tanzanite Marathon, akieleza kuwa mbio hizo ni sehemu ya jitihada za kuchangia moja kwa moja katika kuokoa maisha ya watoto njiti.

Manyara Tanzanite Marathon 2026 inalenga kukusanya jumla ya shilingi bilioni 1.5, fedha zitakazotumika katika ujenzi na uwezeshaji wa wodi maalum kwa ajili ya kutoa huduma kwa watoto wanaozaliwa kabla ya wakati.

Mbio hizo zimewakutanisha wananchi na wanariadha kutoka maeneo mbalimbali, katika kuunga mkono juhudi za kuboresha huduma za afya na kuokoa maisha ya watoto njiti.




































 

No comments: