NGULI WA RIWAYA MOHAMED S. MOHAMED NA ADAM SHAFI KUPAMBA KONGAMANO LA KISWAHILI ZANZIBAR
Njoo umwone, umsikilize, uongee naye, umshike mkono na upige picha naye mwandishi maarufu wa riwaya za Kiswahili ikiwemo Nyota ya Rehema na Kiu: Mohamed Suleiman Mohamed katika Kongamano la Pili la Kimataifa la Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA), mjini Zanzibar Desemba 12 na 13 mwaka huu.
Riwaya ya kwanza ya mwanariwaya Adam Shafi ilikuwa KULI lakini siku ya Kongamano atakizindua kitabu Kuona Mtoto wa Mama. Fika umwone, umshike mkono,muongee na kupiga picha naye.Bahati ilioje! Ni Desemba 12 na 13 mwaka huu.




No comments: